ARISE II:
Mradi wa Kutokomeza utumikishwaji wa watoto kwa jamii wanaojishughulisha na
ulimaji wa zao la Tumbaku unaotekelezwa kijiji cha Migungumalo kilichoko wilaya
ya Uyui mkoani TABORA – TANZANIA
Mkataba wa kuanza mradi : Tarehe ya kuanza: 22nd May 2017 hadi 15 nd
August 2017
Thamani ya Mradi: Tshs 33,484,500/=
Shirika
la Spiritual Life In Christ(SLIC) ni shirika la kidini liliosajiliwa mwaka 2002
kama shirika la kijamii.
Dira yetu ni kuona jamii
inafanikiwa kimwili na kiroho kwa pamoja
Dhima ama Lengo la shirika hili kuhakikisha
jamii inaendelea katika nyanja zote kupitia fikra za maisha ya kimwili na
kiroho bila ubaguzi wa rangi, dini,
jinsi, umri na hali zote za kiubaguzi
Mratibu wa Mradi Ndg Makala Mohamed |
SLIC
imekuwa ikifanya miradi mbalimbali
mashirika ya kitaifa,kimataifa namakamouni mbalimbali tangu kuanzishwa
kwake mwaka 2002 katika miradi ya mazingira, mapambano ya
UKIMWI na magonjwa mengine, haki za binadamu, ujasiriamali, kutetea watoto na
wanawake, elimu ya demokrasia na uchaguzi, miradi ya elimu na makundi mengine.
Mnamo
22/05/2017 SLIC ilifanikiwa
kupata ufadhili wa mradi wa chini ya Shirika la Kazi Duniani (ILO)
uitwao Kutokomeza
utumikishwaji wa watoto kwa jamii wanaojishughulisha na ulimaji wa zao la
Tumbaku uliotekelezwa kijiji cha Migungumalo kilichoko wilaya ya Uyui mkoani
TABORA – TANZANIA
MALENGO
1. Kutoa elimu
katika jamii inayohusu tatizo la kutumikisha watoto katika shughuli za
uzalishaji wa zao la Tumbaku
2. Kuwatafuta ama kuwabaini watoto walioathirika na
kutumikishwa katika shughuli za Tumbaku mashambani
WALENGWA/
WAFAIDIKA WA MRADI
1.
WA MOJA KWA
MOJA
Wapokeaji wa moja kwa moja
walikuwa kama ifuatavyo: -
1. Kutambuliwa umri wa 12-17 = 120
2. Viongozi wa Serikali na Kijiji na kata na kamati za ulinzi za Watoto (VVCC, VCLC, DSWO, viongozi wa maendeleo ya Kijiji)
3. Viongozi wa kidini
4. Walimu (2).
7. Watu wa kujitolea wa Jumuia na
8. Timu ya Ulinzi ya Watoto Wilaya (DCPT) 5
1. Kutambuliwa umri wa 12-17 = 120
2. Viongozi wa Serikali na Kijiji na kata na kamati za ulinzi za Watoto (VVCC, VCLC, DSWO, viongozi wa maendeleo ya Kijiji)
3. Viongozi wa kidini
4. Walimu (2).
7. Watu wa kujitolea wa Jumuia na
8. Timu ya Ulinzi ya Watoto Wilaya (DCPT) 5
JUMLA
YAO NI 186
Watoto wa Kike walioibuliwa kwenye mradi |
2.
WASIO
WA MOJA KWA MOJA
Wakazi wa Kijiji cha Migungumalo
zaidi ya 500 walipata elimu hii kutoka kwa kamati na viongozi wa serikali na
wadau waliohudhuria semina ya mradi wetu
Hivyo
zaidi ya wanajamii 618 wamefaidika na mradi huu
sawa na lengo la la SLIC katika kutekeleza mradi huu
NJIA ZILIZOTUMIKA KUFANIKISHA MALENGO YA MRADI
1. Kufanya
mafunzo
2. Kuunda kamati
ya kijiji ya kuwalinda na kuwaibua watoto
3. Kusambaza
vipeperushi na tisheti na khanga zenye ujumbe wa mapambano dhidi ya utumikwashi
watoto kwenye mashamba ya tumbaku
4. Mchezo wa
mpira
MATOKEO
MATOKEO
CHANYA
1. Uelewa
umeongezeka kwa jamii kuhusu madhara ya kutumikisha watoto Mashambani na kujua
haki za watoto kwa ujumla hasa suala la kupata elimu, kulindwa, kupendwa na
kuthaminiwa
2. Mwitikio
chanya wa walengwa katika kuhudhuria mafunzo haya
3. Watoto hao 94
waliopatikana waliweza kukusanywa pamoja kwa mahojiano kidogo kukusanya taarifa
zao kasha kukabidhi taarifa zao kwenye mamlaka za serikali na shirika lisilo la
kiserikali la JIDA kwa kutekeleza mradi wa kuwaendeleza na kuwasaidia.
4. Wajumbe 38
(28 me, 10 ke) walioelimishwa juu ya Tatizo hili walisaidia kutoa ushirikiano
kupatikana kwa watoto 94 (41me, 43ke) walioathirika toka katika jamii za
wanaozalisha zao la Tumbaku
5. Kupata
wawakilishi toka vitongoji saba vinavyounda kijiji cha Migungumalo na Baadae
kuwaelimisha juu ya tatizo hili.
6. Wakulima
walielewa madhara ya kazi ya watoto
7. Uundaji
wa kamati kupambana na tatizo na sasa ni kazi.
Uelewa wa kujua haki za binadamu
kwa watoto na watu wazima kwamba haki za binadamu hasa kwa watoto zinapaswa
kulindwa.
Watoto wa kiume walioibuliwa ambao walicheza mpira siku ya mwisho ya mradi kijijini Migungumalo |
MATOKEO
HASI TULIYOBAINI ENEO LA MRADI
1.
Tuligundua uwepo wa matokeo ya
mimba za utotoni kwa wasichana chini ya miaka 18 kwa sababu ya sekta ya
tumbaku.
2.
Umasikini kwa jamii ulifanya
kuwatumikisha watoto kama nguvu kazi ya kujiingizia kipato
3.
Watoto kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya
Afisa Ufuatiliaji na Tathmini wa Asasi ya SLIC Bw. Eric Samuel |
4.
Kupoteza mipango ya shule kwa
watoto, kuongezeka kwa watoto ambao hawana kukamilisha shule, kuongezeka kwa
watoto ambao wanakamaliza masomo bila kujua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu
CHANGAMOTO
1. Kulikuwa na
changamoto kidogo kutoka kwa viongozi wa kijiji wachache waliotaka kulipwa
kiasi kikubwa cha fedha kuliko kile kilichotengwa kwenye bajeti.
2. Kulikuwa na
woga kidogo katika kutoa ushirikiano kwa kuhofia kukamatwa na mamlaka za
kisheria kwa waliokuwa wanawatumisha watoto.
3. Uwepo
wa mila mbaya jadi na desturi
zinazoathiri kundi moja au lingine kupata fursa inayostahili kwa
maendeleo yake na jamii kwa ujumla
4. Kutokuwepo
na tofauti ya Usawa wa kijinsia ambapo wanaume wanahusishwa zaidi ya wanawake
5. Kukosekana
elimu ya msingi kwa watu wazima ni kikwazo cha maendeleo na mwamko wa kujua
haki na wajibu wao katika jamii zao.
MAONI
1.
Elimu hii iendelee zaidi ili Jamii isijisahau
ikawatumisha watoto kwa shughuli za kilimo ikiwa ni pamoja na watoto wenyewe
kujitambua haki zao za Elimu na afya
2.
Viongozi wa serikali wanapaswa kuelimishwa umuhimu wa
miradi hii kwa jamii na umuhimu wa kushiriki kwa nafasi zao kamaviongozi wa
serikali eneo la mradi
3.
Elimu ya jinsia ihamasishwe maeneo ya vijijini ili
kuondoa mfumo dume na kandamizi na unyanyasaji kwa makundi mengine
4.
Elimu ya afya na afya ya uzazi itolewe na kusisitizwa
maeneo ya vijijini ilikupambana na mimba za utotoni na madhara ya magonjwa
mengine kwa jamii.
ASANTENI
MRATIBU WA
MRADI SLIC.
17/12/2017