Asasi ya Spiritual Life In Christ (SLIC) ni asasi ya kidini
iliyopo mkoani tabora yenye lengo la kuona jamii inafanikiwa kimwili na
kiroho katika Nyanja ya maendeleo.
Asasi hii imekuwa ikifanya miradi mbali mbali ya ikiwemo
mapambanio dhidi ya ukimwi, malaria, mazingira, ukatili wa kijinsia, miradi ya
nyuki.
![](file:///C:/Users/MAK/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg)
Figure 1 Mratibu wa Mradi Bw Makala Mohamed akitoa
mafunzo kwenye mradi wa Kutokomeza Utumikishwaji wa Watoto kwenye jamii za
wakulima wa Zao la Tumbaku kijiji cha Migungumalo wilaya ya Uyui mkoani Tabora
Akiongea na gazeti hili afisa Mradi huu Bwa Momahed Makala
alisema ,mradi huu unalenga kuwaibua watoto waliokosa fursa na haki zao kama
watoto kutokana na shughuli za kilimo cha tumbaku katika kijiji cha Migungumalo
Wilayani Uyui.
Mwezi Mei , 2017 asasi ya SLIC ilipata fursa ya kufanya
mradi wa Utokomezwajai wa Utumikishwaji
wa watoto kwenye Jamii ya wakulima wa zao la Tumbaku katika kijiji cha
Migungumalo ulifadhiliwa na Shirika la Kazi Duniani (ILO) kiasi cha shilingi 33,494,500.00/= kilitolewa
ili kutekeleza mradi huo.
Uwepo wa timu imara
ya wafanyakazi wa ILO, SLIC , Viongozi wa serikali, Jamii ya Wakazi wa
Migungumalo na uundwaji wa kamati ulipelekea kuibuliwa kwa watoto 94 waliokuwa wakitumikishwa katika mashamba ya
tumbaku.
![](file:///C:/Users/MAK/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image004.jpg)
Figure 2 Watoto wakike walioibuliwa kipindicha mradi wa
Utokomezwaji wa utumikishwaji kwa watoto kwenye jamii ya wakulima wa zao la
tumbaku kijiji cha Migungumalo Uyui-Tabora
Naye afisa
ufuatiliaji na Tathmini wa SLIC Bwa Eric Samuel alisema Kati ya hao 94
walioibuliwa kwenye utumikishwaji wa kilimo cha tumbaku wavulana ni 62 na wasichana ni 32; Watoto 13
walirejeshwa shuleni na wengine walozidi umri wa kusoma walipatiwa mafunzo yakiwemo ya useremala, ufundi ujenzi, ufugaji
wa kuku, kilimo cha mbogamboga naujasiriamali.
![](file:///C:/Users/MAK/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image006.jpg)
Figure 3 Afisa Ufuatiliaji na Tathmini
wa Asasi ya SLIC Bw. Eric Samuel
Aidha mradi umebaini uwepo wa magonjwa ya macho kwa watoto ,
ugonjwa wa kifua na ugonjwa wa ngozi
ambao unatokana na kemikali ama madawa yanayotumika katika kuua wadudu kwenye
mimea ya tumbaku kuwaathiri baadhi ya watoto hao
![](file:///C:/Users/MAK/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image007.jpg)
Figure 4 Mgeni Rasmi Bw Mohamed Shauri akiongea siku ya
Michezo yaMradi wa Utokomezwaji wa Utumikishwaji watoto kwenye Jamii za
wakulima wa zao Tumbaku kijiji cha Migungumalo Wilayaya Uyui mkoani
Tabora
Mradi huu ulihitimishwa kwa mchezo wa mpira wa miguu kwa watoto
walioibuliwa kwenye mradi huu katika kijiji cha Migungumalo ambapo timu A iliifunga timu B 2-1 . Mchezo
huu uliongozwa na ujumbe usemao “Tuseme
Hapana kwa Utumikishwaji wa watoto na NDIYO kwa elimu bora wa watoto wetu”
uliokuwa kwenye jezi za mpira na tisheti pamoja na vitenge .
![](file:///C:/Users/MAK/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image009.jpg)
Figure 5 Watoto walioibuliwa kwenye mradi wa kupambana na
utumikishwaji kweli jamii ya wakulima wa zao la tumbaku kijiji cha Migungumalo
Wilaya ya Ujui
Wananchi waliufurahia mradi huu na kuomba uendelee kwenye
vijiji vingine ili kuwasaidia watoto kutoka kwenye shughuli za kilimo cha
tumbaku.
No comments:
Post a Comment